Saturday, 25 June 2016
Neema ya Ajira kushuka Jijini Mwanza
Mkoa wa Mwanza unatarajia kutengeneza fursa za ajira milioni 1.5 ndani ya kipindi cha miaka 20 ijayo baada ya kukamilisha utekelezaji wa mpango wa jiji la Mwanza.
Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, Mwanza inakadiriwa kuwa na watu zaidi ya 800,000.
Idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka hadi kufikia watu 2.4 milioni ifikapo mwaka 2035.
Akiwasilisha rasimu ya mwisho ya mpango huo katika kikao cha wadau wa maendeleo jijini Mwanza, mtaalamu na mratibu wa mradi huo, Ketan Kulkarni amesema mpango huo utatoa dira na mwongozo wa matumizi endelevu ya ardhi na maendeleo ya jiji hilo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment