Saturday, 25 June 2016
Kenya na Ethiopia zakubaliana ujenzi wa bomba la mafuta
Kenya na Ethiopia zimekubaliana kujenga bomba la mafuta litakaloanzia katika pwani ya Kenya na kuelekea hadi mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa.
Kuna mpango wa kujenga bandari kubwa mjini Lamu lakini ujenzi huo umekuwa ukifanywa polepole.
Ethiopia ambayo haina bahari iko tayari kupunguza utegemeaji wake wa bandari ya Djibout ambayo ni mojawapo ya bandari ghali duniani.
Uganda hivi majuzi ilijiondoa katika makubaliano na Kenya mafuta yake yapitie nchini humo.
Kampuni iliyopewa kanadarasi ya ujenzi wa bomba hilo la Uganda iliamua lipitie nchini Tanzania kutokana na ukosefu wa usalama nchini Kenya ambako kuna mashambulizi ya mara kwa mara yanayotekelezwa na wapiganaji wa al-Shabab.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment