Ndege ya kivita ya jeshi la Syria imeanguka muda mfupi baada ya kuruka katika uwanja wa ndege wa Hama. Chanzo cha kijeshi kimesema hitilafu za kiunfundi ndio chanzo cha ajali hiyo. Hata hivyo chanzo hicho, ambacho kimenukuliwa na chombo cha habari cha serikali cha Syria hakijaeleza ajali hiyo imetokea wapi au kutoa maelezo zaidi.
Ndege kadhaa za kijeshi zilizotengenezwa Urusi zimekuwa zikiangkua tangu mwanzoni mwa mwaka huu kutokana na hitalifu za kiufundi jambo ambalo wataalamu wanasema linatokana na uchakavu. Duru kwa upande wa uasi zililiambia shirika la habari la Uingereza Reuters kwamba ndege iliyoanguka ni aina ya Mig 21 jambo ambalo halijaweza kuthibitishwa.
No comments:
Post a Comment