Monday, 20 June 2016
Raia nane wa Syria wauawa mpakani mwa Uturuki
Makundi ya wanaharakati yanasema kuwa wakimbizi wanane raia wa Syria waliuawa kwa kupigwa risasi na walinzi wa mpaka wa Uturuki walipojaribu kuvuka mpaka kwenda nchini Uturuki siku ya Jumamosi usiku.
Wengi wa waathiriwa wanaripotiwa kutoka familia moja wakiwemo wanawake na watoto.
Jeshi la Uturuki limekana kuwaua wakimbizi na kusema kuwa walinzi walifyatua tu risasi za kutoa onyo.
Shirika moja la uchunguzi lenye makao yake nchini Syria, linasema kuwa hadi raia 60 wa Syria wameuawa mwaka huu wanapojaribu kuvuka kuingia Uturuki.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment