Sunday, 26 June 2016

Mhandisi Kakoko ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Bandari Tanzania


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, leo amemteua Mhandisi Deusdedit Kakoko kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Mhandisi Kakoko anachukua nafasi iliyoachwa na Ephraim Mgawe ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Kabla ya uteuzi, Mhandisi Kakoko alikuwa Meneja wa Miradi kutoka Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads).

No comments:

Post a Comment