Saturday, 18 June 2016
Kampeni za kura ya maoni zasimama Uingereza
Zikiwa zimesalia siku sita kabla ya kuitishwa kwa kura ya maoni pande zinazohasimiana ambazo zinapiga kampeni kuu nga mkono kujiondoa au kubaki kwa Uingereza katika Umoja wa Ulaya zilisimasha kampeni zake hizo na wanasiasa nao wameungana kupinga mauaji hayo.
Hata hivyo wachambuzi wamehoji iwapo muuaji anaweza kuchochewa na maudhui ya kampeni hizo ambazo zimekuwa zikiendelea ambazo zimeibua mvutano mkubwa kwa kugusia masuala ya kitambulisho cha kitaifa pamoja na masuala ya uhamiaji.
Gazeti la Times nchini humo limeripoti kuwa Cox ambaye anakuwa mbunge wa kwanza kuuawa tangu mwaka 1990 amekuwa akiandamwa na ujumbe wa vitisho uliotumwa kwake katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita. Kwa mujibu wa gazeti hilo polisi nchini humo walikuwa wakifikiria kuweka ulinzi wa ziada na kuongeza kuwa kulikuwa hakuna uhusiano na ujumbe huo uliotumwa na tukio hilo la mauaji hapo .
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment