Saturday, 18 June 2016
Waziri Mkuu Cameron ashtushwa kifo cha Mbunge
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron naye pia ameshtushwa na tukio la mauaji ya mwanasiasa huyo akisema haya ni maafa makubwa na ni habari za kushitusha. Ametoa rambirambi kwa mume wa mawanasiasa huyo Brendan, watoto wake wawili na familia yake kwa ujumla. Cameron amesema Uingereza imempoteza mwanasiasa na mbunge ambaye alikuwa hodari katika masuala ya kampeni na akifanya hivyo kwa moyo wake wote na kuwa watu wameshitushwa na mauaji hayo.
Awali watu kadhaa waliokuwa na nyuso za majonzi walikusanyika nje ya jengo la bunge la nchi hiyo katika hafla ya kumkumbuka mwanasiasa huyo, tukio ambalo limehudhuriwa pia na kiongozi wa chama cha Labour, Jeremy Corbyn.
Cox ambaye alichaguliwa kuwa mbunge mwaka jana tayari alikuwa amejijengea umaarufu kutokana na jitihada zake za kuishawishi serikali ya nchi hiyo kufanya zaidi katika kuwasaidia wakimbizi wanaotokea nchini Syria na pia kampeni yake ya kuhamasisha Uingereza kuendelea kubakia katika Umoja wa Ulaya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment