Thursday, 16 June 2016
China yaipa onyo Marekani kuhusu Tibet
China imeionya Marekani kukoma kuingilia masuala ya ndani ya nchi yake kwa kutumia suala la Tibet baada ya rais wa Marekani Barack Obama kukutana na kiongozi wa kiroho mwenye ushawishi mkubwa wa watu wa Tibet Dalai Lama katika ikulu ya Marekani. Onyo hilo la China limetolewa na msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa China Lu Kang.
Kadhalika wizara hiyo ya mambo ya nje ya China imesema kwamba njama zozote za kutaka kulitumia suala la Tibet kuingilia mambo ya ndani ya taifa hilo itahujumu usalama wa taifa hilo na mshikamano wa kimadhehebu hautofanikiwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment