Thursday, 16 June 2016

Urusi kusitisha mapigano kwa saa 48 Syria

Urusi imetangaza katika dakika za mwisho usitishwaji mapigano kwa muda wa saa 48 katika mkoa ulioharibiwa vibaya na vita wa Aleppo hapo jana usiku ikiwa ni saa chache baada ya serikali ya Marekani kumuonya rais Bashar al Assad na mshirika wake huyo Urusi kwamba wanabidi waheshimu makubaliano ya kitaifa ya kusitisha vita yaliyofikiwa mwezi Februari. Mkoa huo muhimu wa kaskazini mwa Syria wa Aleppo umekumbwa na mapigano makali na kuharibiwa kabisa katika vita vilivyosababisha vifo vya zaidi ya watu 280,000. Taarifa za shirika linalofuatilia hali ya haki za binadamu la Syria lenye makao yake London Uingereza zinasema wapiganaji kadhaa wameuwawa katika mapigano mapya kati ya vikosi vya serikali, waasi na wapiganaji wa jihadi kusini mwa mji wa Aleppo jana. Hata hivyo tangazo la Urusi la kusitisha vita kwa siku mbili halikutoa ufafanuzi nchi hiyo imejadiliana na nani kuhusiana na hatua hiyo.

No comments:

Post a Comment