Wednesday, 22 June 2016

Ahukumiwa miezi 9 baada ya kutembea toka Ufaransa hadi Uingereza


Mwanaume mmoja raia wa Sudan amehukumiwa kifungo cha miezi tisa jela na mahakama moja nchini Uingereza baada ya kupatikana na hatia ya kutembea kwa miguu kutoka nchini Ufaransa hadi Uingereza akifuata kwa reli.

Abdul Rahman Haroun, ambaye alikiri mashtaka hayo alikuwa amepewa hifadhi nchini Uingereza mwaka uliopita.

Mwanamme huyo wa umri wa miaka 40 anaaminika kutembea umbali wa kilomita 50 kutoka Calaisin nchini Ufaransa, hadi Folkestone nchini Uingereza kabla ya kupatikana tarehe 4 mwezi Agosti mwaka uliopita.

Hata hivyo hawezi kufungwa jela kutoka na kipindi ambacho tayari amekuwa kizuizini.

1 comment: