Thursday, 16 June 2016

Wakurugenzi kubanwa mbavu kuhusu mikopo ya wanawake na vijana


Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imesema itaanza kuwashughulikia wakurugenzi wa halmashauri ambao hawatoi asilimia 10 ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanawake na vijana.

 Hii si mara ya kwanza kwa ofisi hiyo kutoa maagizo hayo licha ya utekelezaji wake kuwa mdogo.

 Mwaka 2013, aliyekuwa Naibu Waziri wa Tamisemi, Aggrey Mwanri alitoa tamko kama hilo.

 Jana, Naibu Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Sikudhani Chikambo (CCM), amesema ni marufuku kwa halmashauri yoyote kutumia asilimia 10 iliyotengwa kwa ajili ya wanawake na vijana.

No comments:

Post a Comment