Thursday, 16 June 2016
Wafanyabiashara wapunguza ujazo wa Sukari
Mbeya. Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA), Mkoa wa Mbeya, Deogratius Hussein amesema wafanyabiashara wa sukari wamekuwa wakipunguza ujazo kutoka kilo moja hadi gramu 700.
Amesema msako unaendelea kupambana nao na kwamba watatu wamekamatwa huku mmoja akifikishwa kortini na wawili kutozwa faini ya Sh300,000 kila mmoja.
Tayari kilo 1,150 za sukari zimeingia mkoani humo kutoka nchini Malawi kwa lengo la kupunguza upungufu wa bidhaa hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amesema anaamini tatizo la ukosefu wa sukari litakwisha, kwani hadi sasa tani 130 zimeingia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment