Saturday, 18 June 2016
Wakenya wakoshwa na Rais Magufuli
Makamu mkuu wa Shule Kuu ya Biashara ya Strathmore (SBS) ya jijini Nairobi, Dk Vincent Ogutu amesema Wakenya wamefurahi kuona namna Rais John Magufuli anavyopinga ufisadi kwa kusimamia sheria.
Akizungumza kwenye mkutano wa Watendaji Wakuu wa Kampuni Binafsi (CEOrt) juzi, amesema Serikali zina sheria nyingi nzuri, lakini hazina viongozi wenye uwezo wa kuzisimamia ipasavyo.
Amesema anatamani kuona nchi za Afrika Mashariki zinapata aina moja ya mafunzo ya uongozi kwa kuwa tofauti nyingi zilizokuwapo awali zimeondolewa.
Mkurugenzi wa SBS, Dk George Njenga amesema upo umuhimu kwa viongozi kufundishwa maadili ili waondokane na tabia ya kuwajengea hofu wananchi.
Labels:
Habarii za Kisiasa
Location:
Nairobi, Kenya
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment