Saturday, 18 June 2016

Wakenya wakoshwa na Rais Magufuli


Makamu mkuu wa  Shule Kuu ya Biashara ya Strathmore (SBS) ya jijini Nairobi, Dk Vincent Ogutu amesema Wakenya wamefurahi kuona namna Rais John Magufuli anavyopinga ufisadi kwa kusimamia sheria.

Akizungumza kwenye mkutano wa Watendaji Wakuu wa Kampuni Binafsi (CEOrt) juzi, amesema  Serikali zina sheria nyingi nzuri, lakini hazina viongozi wenye uwezo wa kuzisimamia ipasavyo.

Amesema anatamani kuona nchi za Afrika Mashariki zinapata aina moja ya mafunzo ya uongozi kwa kuwa tofauti nyingi zilizokuwapo awali zimeondolewa.

Mkurugenzi wa SBS, Dk George Njenga amesema upo umuhimu kwa viongozi kufundishwa maadili ili waondokane na tabia ya kuwajengea hofu wananchi.

No comments:

Post a Comment