Saturday, 18 June 2016

Pigo jingine tena kwa Wabunge wa Upinzani


Wabunge wawili wa Viti Maalumu wa Chadema, Suzan Lyimo na Anatropia Theonest wamesimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa  kusema uongo bungeni.

Naibu Spika, Dk Tulia Ackson amesema  bungeni Dodoma jana kuwa  kwa kutumia Kanuni ya 63 (8) ya Kanuni za Kudumu za Bunge toleo la Januari 2016, ameridhia mapendekezo ya taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge iliyowatia hatiani wabunge hao baada ya kuwahoji na kushindwa kuthibitisha madai yao.

Katika adhabu hiyo ,  Lyimo amesimamishwa kuhudhuria vikao vitano kuanzia jana hadi Juni 24, huku Theonest akisimamishwa kuhudhuria vikao vitatu kuanzia jana hadi Juni 22.

Wawakilishi hao pia, hawataruhusiwa kuingia viwanja vya Bunge na watakatwa nusu ya mishahara yao na posho kwa kipindi watakachokuwa wakitumikia adhabu hizo, kwa mujibu wa masharti ya kanuni ya 75 za Kanuni za Kudumu za Bunge.

No comments:

Post a Comment