Tuesday, 28 June 2016
Vituo vya mafuta Nchini Kenya vyanyang'wa leseni
Tume ya kudhibiti nishati nchini Kenya (ERC), imevipokonya leseni vituo vya mafuta kwa kuuza mafuta machafu.
Uchunguzi uliofanywa ulibaini kuwa mafuta ya diesel na petroli, yalikuwa yamechanyanywa na mafuta taa pamoja na bidhaa zingine.
Hata hivyo ni vituo vichache viliathiriwa kwa sababu asilimia 96.1 ya vituo vyote vilivyofanyiwa uchunguzi viligunduliwa kuwa na mafuta safi.
Tume hiyo ilianzisha mpango wa kuchunguza mafuta mwaka 2015 ili kuwawezesha wauza mafuta, kuhakikisha kuwa mafuta yao ni safi kabla ya kuyauza.
Labels:
Madini na Nishati
Location:
Nairobi, Kenya
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment