Thursday, 30 June 2016

Uwanja wa Ndege watwaliwa na Waasi nchini Syria


Wapiganaji wa waasi wa Syria wanaosaidiwa na Marekani walichukua udhibiti wa uwanja mdogo wa ndege uliotumika kama kambi na kundi la Islamic State karibu na mpaka wa Irak mapema hapo jana.

Kambi ya jeshi la anga huko Hamdan ilitumika kama kituo muhimu cha kijeshi cha Islamic State karibu na mji wa Al-Bukamal, kilomita chache kutoka Irak.

Kambi hiyo ya jeshi la anga ilitekwa saa kadhaa baada ya kuanzishwa mashambulizi siku ya Jumanne yaliyokuwa na lengo la kufunga njia inayotumiwa na kundi la ugaidi kuingia Syria na Irak.

Kundi la Islamic State lilichukua udhibiti wa Al-Bukamal mwaka 2014 kwa ajili ya operesheni zao za kijeshi na mara moja kuondoa mpaka kati ya Irak na Syria.

No comments:

Post a Comment