Tuesday, 28 June 2016

Rais JPM hula chakula alichopika Mama Janette Magufuli


Baada ya kutambuliwa kama mtu mwenye msimamo mkali na asiyependa dhihaka, mabaye huwafuta watu hadharani, huenda sasa Rais wa Tanzania John Magufuli ana maadui wengi.

Sasa akiwa Ikulu na kama njia ya kuchukua tahadhari, inaripotiwa kuwa Magufuli hula chakula kilichopikwa na mke wake tu.

Kulingana na gazeti la Financial Times ni kwamba hili limedhihirika kutoka na upinzani anaokumbana nao.

Lakini hilo halijathibitishwa bado wala gazeti la Financial Times halijasema ni jinsi gani walipata uvumi huo.

No comments:

Post a Comment