Tuesday, 28 June 2016
Tume ya Uchaguzi yawasilisha Taarifa za Uchaguzi wa Zanzibar
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi –NEC Jaji mstaafu Damian Lubuva amesema amefarijika kuona Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 umemalizika katika hali ya usalama na amani.
Jaji Lubuva amesema hayo kisiwani Zanzibar alipokuwa akikabidhi taarifa ya mwenendo wa uchaguzi kwa Spika wa Baraza la wawakilishi .
Akizungumzia suala la Katiba mpya iliyopendekezwa Jaji Lubuva amesema atahakikisha anasimamia sheria ambazo zimepitwa na wakati kwa lengo la kutetea haki za wananchi.
Naye Spika wa Baraza la wawakilishi Kisiwani Zanzibar Zubeir Ali Maulid amemshukuru Jaji Lubuva kwa kutembelea baraza hilo na kusema wakazi wa Zanzibar wanaendelea kuishi katika hali ya amani na usalama.
Labels:
Habari za Kisiasa
Location:
Zanzibar, Tanzania
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment