Tuesday, 28 June 2016

KMKM yawazuia watetezi wa Haki za binadamu


Kikosi maalum cha kupambana na magendo, KMKM, kisiwani Pemba kimewazuia ndugu, jamaa na watetezi wa haki kukaribia mahakama ya Wete, Mkoa wa Kaskazini kwa kile walichodai ni maelekezo kutoka ngazi za juu.

Tukio hilo lilitokea wakati wananchi kadhaa wakishikiliwa kwa tuhuma za kujihusisha na uharibifu wa mashamba na mali mbalimbali za makada wa Chama cha Mapinduzi kisiwani Pemba.

Kutaka kufahamu zaidi kuhusu kinachoendelea Josephat Charo amezungumza na Mkurugenzi wa Haki za Binaadamu wa chama cha Wananchi, CUF, Pemba, Mwinyi Juma.

No comments:

Post a Comment