Friday, 17 June 2016
Poland kuinua kilimo cha Tanzania kwa kuipa matrekta
Tanzania kupata matrekita ya kilimo kutoka Poland
Kampuni moja inayohusika na utengenezaji wa matireketa ya kilimo ya Ursus ya nchini Poland imetiliana saini na Shirika moja la kujenga Taifa la nchini Tanzania kwa ajili ya kusambaza jumla ya matrekita 2,400, pamoja na zana nyingine za kilimo na vipuri nchini humo. Kampuni hiyo ambayo pia imekuwa ikifanya biashara na Ethiopia inaendelea na mazungumzo kwa ajili ya usambazaji wa zana hizo za kilimo katika mataifa ya Angola na Nigeria. Mauzo ya nje ya Poland kwa mataifa ya bara la Afrika yanakadiriwa kufikia thamani ya dola bilioni 4.5, likiwa ni ongezeko la karibu kiwango cha asilimia 20 kwa mwaka.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment