Tuesday, 21 June 2016

Mtu aliyevaa mkanda bandia ametishia kujiripua leo mjini Brussels


Mtu  aliyesema  amevaa  mkanda  wa  mabomu  ambao ungeripuka  kwa  kufyatuliwa  kwa  mbali  amesababisha kitisho  kikubwa  katika  eneo  la  kibiashara  mjini  Brussels leo kabla  ya  polisi  kugundua  kwamba  mkanda  huo ulikuwa  na  chumvi  na  biskuti ndani yake.

Jiji  la  Brussels  limeendelea  kuwa  katika  tahadhari  chini ya  ulinzi  mkali  miezi  mitatu  baada  ya  washambuliaji watatu  wa  kujitoa  mhanga  wa  kundi  la  Dola  la Kiislamu  walipojiripua  katika  uwanja  wa  ndege  wa  mjini Brussels  na  katika  kituo  cha  treni  na  kusababisha watu 32  kuuwawa.

Leo asubuhi  polisi  wa  mjini Brussels  walimkamata  mtu mmoja  karibu  na  eneo  la  maduka  baada  ya  kusema kuwa  alikuwa  amevaa  mkanda  wa  miripuko. Eneo  hilo lilifungwa  wakati  wataalamu  wa  mabomu  wakimpekua mtu  huyo.

Mtu  huyo  aliyezaliwa  mwaka  1990  na  kutambulika kwa jina  la  J.B aliwapigia  simu  polisi  binafsi  na  kusema ametekwa  nyara  na  kulazimishwa  kuvaa  mkanda  wenye miripuko. Imethibitika  kwamba  si  kweli.

No comments:

Post a Comment