Tuesday, 21 June 2016
Jumla ya Madaktari 700 waliuawa nchini Syria tangu mzozo ulipoanza
Mashambulio dhidi ya hospitali tangu vita nchini Syria vianze miaka mitano iliyopita yameuwa madaktari pamoja na wafanyakazi wa kutoa huduma za afya 700, wengi wao kwa mashambulizi ya anga.
Tume ya Umoja wa Mataifa ya uchunguzi kuhusu Syria pia imeshutumu ukiukaji mkubwa unaofanywa na wapiganaji wa Jihad na kueleza wasi wasi wake kwamba wanamgambo wenye mafungamano na Al-Qaeda huenda wanawaandikisha mamia ya watoto katika vikosi vyao.
Kamishna Paulo Pinheiro ameliambia baraza la haki za binadamu la Umoja wa mataifa kwamba mashambulio yenye malengo maalum ya anga dhidi ya hospitali na kliniki nchini Syria, yamesababisha vifo vya raia kadhaa, ikiwa ni pamoja na wafanyakazi muhimu wa huduma za afya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment