Saturday, 25 June 2016
Dar waupongeza Uongozi Muhimbili kwa kutoa chakula
Baada ya Juni 21 Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuanza utaratibu mpya wa kutoa chakula kwa wagonjwa kuanzai Julai 1, wananchi wa wa jiji la Dar es Salaam wamedai kuwa kitu hiko kitawezekana kama kitasimamiwa ipasavyo.
Wakati akitangaza agizo hilo kwa niaba ya uongozi wa hospitali ya Muhimbili, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaesha alisema kuwa utaratibu huo mpya, watatoza Sh 50,000 pindi watakapompokea mgonjwa, ambazo Sh 10,000 zitakuwa ni kwa ajili ya kitanda, Sh 10,000 ya kumuona daktari na Sh 30,000 itakuwa ni chakula kwa siku zote atakazokuwepo mgonjwa hospitali.
Alisema wamejipanga kutoa huduma bora ya chakula ambapo kwa wiki wagonjwa watakula ugali mara tano, wali mara tatu, pilau mara mbili na viazi mara tatu.
Wakiongea kwa nyakati tofauti, mmoja kati ya wananchi wa jiji la Dar es Salaam waliotoa maoni yao kuhusu tukio hilo alisema kuwa tukio hilo siyo mara ya kwanza kutokea hapa nchi kwani miaka ya nyuma serikali iliwahi kufanya kama hivyo lakini baada wakasitisha zoezi hilo.
Labels:
Afya ya Jamii
Location:
Dar es Salaam, Tanzania
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment