Zaidi ya watu 100 wamenusurika kifo baada ya moto kuteketeza kituo cha kulelea watoto cha Faraja kilichopo Mgongo kata ya Nduli manispaa ya Iringa na kusababisha zaidi ya watoto 70 ambao ni wanafunzia wa shule mbalimbali za kituo hicho cha kulelea watoto wa mazingira hatarishi kukosa mahali pa kulala.
Moto huo uliozuka majira ya saa kumi na moja jioni na kudumu hadi saa 11 alfajiri ya leo umeteketeza kabisa jengo la mabweni ya wanafunzi hao huku wenyewe wakiwa wametoka kwaajili ya matembezi hali inayoonekana kama muujiza.
Kufuatia hali hiyo uongozi wa mkoa wa Iringa umefika kujionea uharibifu huo na kutoa misaada mbalimbali yakiwemo magodoro na mabranketi kwaajili ya kusaidia maisha ya watoto wa kituo hicho ambao wameunguliwa na vifaa vyao yakiwemo madaftari pamoja na nguo zao.
Veronica nziku anatoa shukrani kwa mkuu wa mkoa na msafara wake kwa niaba ya wenzake wa kituo hicho ambapo serikali ya mkoa licha ya kukabidhi msaada huo imewaomba watu mbalimbali kujitolea kusaidia kituo hicho kwa lengo la kurejesha maisha ya watoto hao kama yalivyokuwa zamani.
No comments:
Post a Comment