Saturday, 2 July 2016

Waliotekwa mgahawa wa Dhaka waokolewa


Mateka 13 wameokolewa kutoka katika mgahawa wa Dhaka ambapo wapiganaji wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kiislam walikuwa wamewakamata mateka baada ya Makomando wa Bangladesh waliojihami vyema kwa silaha kuvamia eneo hilo leo Jumamosi

Mateka hao ikiwa ni pamoja na wageni watatu , kumi raia wa Bangladesh, wameokolewa baada ya makabiliano makali ya risasi kati yao na polisi, maafisa wamesema.

Mpiga picha wa AFP ambaye yupo katika eneo la tukio amesema aliweza kusikia milio mikubwa ya risasi wakati vikosi vya usalama vilipozindua operesheni ya uokozi zaidi ya saa 10 baada ya wanamgambo hao kuwakamata mateka.

Mateka watano wameokolewa katika dakika chache za kuanza kwaoperesheni hiyo, amesema Tuhin Mohammad Masoud kamanda wa juu wa kikosi cha haraka cha makomando wasomi wa Bangladeshi ambao walivamia mgahawa huo.

No comments:

Post a Comment