Thursday, 7 July 2016

Makosa ya barabarani yaongezeka Mkoani Mwanza


Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabara kimekamata makosa 11, 088 kwa kipindi cha Juni kutoka makosa 10,389 yaliyotokea Mei.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema jana kuwa  kuongezeka kwa idadi ya makosa hayo kumetokana na umakini wa askari wa usalama barabarani katika kudhibiti wavunjaji sheria.

Amesema kutokana na makosa hayo,  wamekusanya zaidi ya Sh329.7 milioni zikiwa ni tozo za faini.

“Hata hivyo, makosa makubwa ya uhalifu yameongezeka Juni kufikia 232, ikilinganishwa na 197 ya Mei,” amesema Msangi.

No comments:

Post a Comment