Saturday, 9 July 2016

Korea Kaskazini yarusha kombora la masafa marefu


Korea Kaskazini kwa mara nyingine imetekeleza jaribio la kombora lake la  masafa marefu kuelekea baharini.

Hili ndilo jaribio la hivi karibuni kutekelezwa na jeshi nchini humo kinyume na wito wa Umoja wa Mataifa pamoja na mataifa jirani kama Korea Kusini na Japan kuitaka kuacha majaribio hayo kwa sababu za kiusalama.

Jaribio hili limefanyika licha ya kuwepo kwa azimio la Umoja wa Mataifa kuzuia nchi hiyo ambayo inaendeleza mpango wa kutengeneza silaha za Nyuklia kwa lengo la kushambulia mataifa ya Magharibi.


Hili ni jaribio  la nne kuwahi kutekelezwa na Pyongyang tangu mwezi Januari mwaka huu wakiwa na lengo la kuwa na silaha za masafa marefu kuishambulia Marekani.

Nchi za Marekani na Korea Kusini zimekubaliana kuweka mpango wa pamoja kutega mitambo maalum kuzuia mashambulizi kama haya katika siku zijazo.

No comments:

Post a Comment