Sunday, 3 July 2016

Beatrice Shelukindo afariki dunia


Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kilindi Beatrice Shellukindo (CCM) ameaga dunia jana Jijini Arusha.

Akithibitisha kifo hicho Katibu wa CCM Wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga, Hawa Nanganyau alisema marehemu  ameugua tangu  mwaka 2014 akisumbuliwa na tatizo la mgongo pamoja na miguu.

Beatrice mpaka anafikwa na umauti alikuwa ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC)  kupitia Wilaya ya Kilindi.

Katibu huyo wa CCM  amesema marehemu ameacha watoto watatu wote wa kiume  na atazikwa siku ya Jumatano saa sita mchana jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment