Wednesday, 29 June 2016
Watatu wauawa na Polisi Tanga
Jeshi la Polisi mkoani Tanga limewahakikishia wananchi kwamba eneo la amboni lipo salama baada ya kuwakamata watuhumiwa watatu, Bunduki 2 aina ya SMG, bastola moja, risasi 30, mapanga na silaha nyingine katika msako maalum ulioshirikisha na vyombo vya ulinzi na usalama.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga Leonard Paulo amesema silaha hizo zimepatikana zikiwa zimefukiwa ardhini ambapo watu waliokamatwa wanaaminika ndiyo waliohusika na mauaji ya watu 8 katika Mtaa wa kibatini.
Kamanda Paulo amesema watuhumiwa hao watatu wamefariki kutokana na majeraha waliyopata katika mapambano na vyombo vya usalama akiwemo kiongozi mkubwa wa kundi hilo ambaye ametambuliwa kwa jina la Abu Seif.
Aidha kamanda Paulo ametoa wito kwa jamii kuendelea kutoa taarifa mbalimbali zitakazowezesha kubaini wahalifu na kuwahakikishia wananchi kuwa eneo la amboni liko salama na limedhibitiwa.
Labels:
Ulinzi na Usalama
Location:
Tanga, Tanzania
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment