Sunday, 26 June 2016
Thelathini wafa kwa ajali China
Watu 30 wamefariki dunia katikati mwa China katika ajali ya basi moja lililoungua moto kufuatia kuanguka pembeni mwa barabara.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari abiria 56 walikuwamo ndani ya basi hilo ambapo majeruhi 21 walikimbizwa hospital kwa matibabu zaidi.
Katika video iliyoonyeshwa na shirika la utangazaji la CCTV, kulionekana moshi mweusi na mzito kutoka katika basi ambapo mamlaka za mji zinasema ajali hyo huenda imesababishwa na kuvuja kwa mafuta baada ya basi hilo kuanguka pembeni mwa barabara.
China inakabiliwa na kiwango kikubwa cha ajali za barabarani ambapo inakadiriwa kuwa watu 250,000 hufariki kila mwaka kutokana na ajali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment