Sunday, 19 June 2016

Mhe. Kikwete na changamoto za Elimu nchini


Jana Rais mstaafu, Mhe. Jakaya Kikwete alisema licha ya upatikanaji wa elimu ya msingi na sekondari ni bure, Serikali pekee haiwezi kutatua changamoto zilizopo.

Kikwete alisema hayo jana wakati wa matembezi ya hisani kwa ajili ya kuchangia gharama za elimu yanayoendeshwa na Taasisi ya Binti Foundation kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.

Kikwete, ambaye aliongoza Serikali ya Awamu ya Nne alisema mtoto anayeishi katika mazingira ya umaskini, elimu bure bado inakuwa ni changamoto kwake kwa ana mahitaji mengi ambayo mzazi anatakiwa ayagharamie ikiwamo chakula, sare za shule na mengine muhimu.

“Mtoto anayehudhuria masomo lakini nguo zake zimechanika, atakuwa darasani, hana furaha atabaki mnyonge tofauti na wenzake. Hapo atashindwa kuitumia ipasavyo haki yake ya msingi ya kupata elimu kutokana na mazingira anayoishi,” alisema.

No comments:

Post a Comment