Thursday, 30 June 2016
Lissu akana mashtaka na kuachiwa kwa dhamana
MBUNGE wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) amesomewa shitaka lake la kutoa maneno ya uchochezi kinyume cha kifungu namba 32 cha sheria ya magazeti.
Lissu anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mnamo June 28, 2016 kwa kumuita ‘Mkuu wa Nchi ni dikteta uchwara’.
Baada ya kusomewa shtaka hilo Lissu amekana shtaka na kuachiwa huru kwa dhamana na hatotakiwa kusafiri nje ya nchi bila kibali cha mahakama.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena Agosti 02, 2016.
Labels:
Haki na Sheria
Location:
Dar es Salaam, Tanzania
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment