Thursday, 23 June 2016

Bandari ya Dar es Salaam yalipuliwa tena, kunani?


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ameapa kusambaratisha mtandao wa kifisadi uliopo Bandari ay Dar es Salaam.

Ameiagiza pia bodi mpya ya Bandari kushughulikia tatizo hilo alilodai kuwa ni kubwa na linahatarisha utendaji kazi wa bandari.

Akizungumza katika uzinduzi wa bodi hiyo jijini Dar es Salaam jana, Profesa Mbarawa alisema kuna baadhi ya kampuni za kupakua mizigo bandari zenye wafanyakazi walioajiriwa na bandari, huku baadhi yao wakiwa wameajiriwa kwa upendeleo.

“Kuna wafanyakazi wengi wa bandari wanaofanya kazi katika kampuni binafsi bandarini. Kuna kampuni (anaitaja) ambayo mume wa mmiliki wake aliyeajiriwa bandari ana hisa asilimia 50, tumefanya uchunguzi lakini Mwanasheria wa Bandari anasema hakuna  conflict of interest (mgongano wa kimaslahi). Mwanasheria gani huyu?” alihoji Profesa Mbarawa na kuongeza:

“Watu wameajiri ndugu zao bandarini, kuna mtu ameajiri ndugu zake saba.

No comments:

Post a Comment