Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene amesema sheria haziwaruhusu viongozi wa umma kuwa na kampuni binafsi zinazofanya kazi ndani ya manispaa wanazoongoza.
Waziri Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Kibwake (CCM), amesema mkurugenzi atakayebainika kutoa zabuni kwa kampuni yake binafsi wakati ni kiongozi wa umma, atachukuliwa hatua za kisheria.
Ametoa kauli hiyo juzi wakati akipokea vifaa vya kisasa likiwamo trekta na mitambo maalumu kwa ajili ya Mradi wa Uboreshaji Miji Kimkakati (TSCP), kutoka kwa Mratibu wa mradi, Davis Shemangali.
“Sidhani kama wapo wenye tabia hii. Kama wapo waache mara moja kujihusisha na mchezo huu kwani tutawachukulia hatua kali,” alisema Waziri Simbachawene.
No comments:
Post a Comment