Saturday, 16 July 2016

Ney wa Mitego ahojiwa na Polisi


Msanii wa muziki wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki maarufu kama  Ney wa Mitego amehojiwa kituo cha Polisi Kati na kupewa dhamana kufuatia tuhuma zinazomkabili.

Kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema msanii huyo alihojiwa juzi kituoni hapo na yupo nje kwa dhamana, huku jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na  tuhuma zinazomkabili.

“Ni kweli juzi mchana  tulimhoji Ney wa Mitego na yupo nje kwa dhamana kuhusu kukamatwa kwake nitatoa taarifa  kwa nini tulimkamata,”amesema Kamanda Sirro.

No comments:

Post a Comment