Saturday, 16 July 2016

Ndessamburo ataka CHADEMA ijengwe


Aliyekuwa mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo amesema inahitajika nguvu kukijenga Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutokana na Serikali kuzuia kufanyika kwa mikutano ya hadhara nchini.

Ndesamburo ambaye ni mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro amesema  wakati akifungua mkutano wa faragha wa  makatibu na wenyeviti wa chama hicho wa wilaya.

“Kujenga chama siyo mchezo, tunakoeleka siyo kuzuri tukaze buti na tutekeleze tunachokisimamia kwa vitendo kwa sababu wenzetu wanatumia mbinu nyingi kuhakikisha wanatukwamisha,” alisema.

Amefafanua kuwa kutokana na chama hicho kuzuiliwa kufanya mikutano ya hadhara, viongozi wa kata hadi Taifa wanatakiwa kuongeza nguvu ya ziada na kutumia mbinu mbadala kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao.

Mratibu wa chama hicho Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa amesema wameamua ‘kutafuna mbuyu’ chini kwa chini kutokana kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara ili kuhakikisha chama hicho hakiyumbi.

No comments:

Post a Comment