Monday, 11 July 2016

Mwanamke apinga unyanyasaji unaotekelezwa na Polisi nchini Marekani


Maandamano nchini Marekani kupinga mauaji ya wanaume weusi na polisi wazungu yameendelea katika mji wa Baton Rouge, Louisiana.

Makumi ya waandamanaji walikamatwa huku polisi wakiendeleza sera yao ya kuwakamata kamata weusi wanaopinga mauaji hayo ya polisi.

Viongozi wa vuguvugu la Black Lives matter walikamatwa
Matukio ya makabiliano hayo yameibua hofu ya kuenea kwa uhasama na ubaguzi wa rangi. Hata hivyo picha moja imeibua hisia kali kwenye mitandao ya kijamii kote duniani.

Polisi wameendeleza kauli ya kuwa na msimamo mkali dhidi ya weusi
Picha hiyo inaonesha maafisa wawili wa polisi waliojihami hadi kwenye kisigino wakijiandaa kumkabili kipusa mmoja mweusi ambaye hakuwa amejihami kwa namna yeyote ila kwa ujasiri wa kupinga mauaji hayo ya wanaume weusi jumanne iliyopita.

Picha hiyo ya mwanamke huyo imefananishwa na ile ya ''Tank Man'' ya China
Picha hiyo ilipigwa na mpiga picha wa shirika la habari la Reuters Jonathan Bachman, ambaye ni mkaazi wa mji wa New Orleans.

Waamerika wengi waliosambaza picha hiyo wameifananisha na ile picha ya mwanaume aliyekuwa akipigania haki za wenyeji nchini China wakati walipokabiliwa na wanajeshi wakiwa wamejihami na vifaru vya kijeshi.

Wapiganiaji haki za kibinadamu na haswa haki za wamarekani weusi wamekuwa wakijadili sadfa ya kuwa taifa linalodai kuwa kitovu cha demokrasia kinatumia mbinu za kidhalimu zilizotumika mataifa ya kikomunisti karne iliyopita.

Wanaume weusi wamejipata pabaya mikononi mwa polisi wazungu
Mpiganiaji haki za weusi Shaun King ambaye pia ni mwandishi wa jarida la New York Daily anasema kuwa ni jambo la kufedhehesha mno mno kuwa picha hiyo ya kihistoria inatokea Marekani mwaka huu wa 2016, weusi wakipigana dhidi ya ubaguzi wa rangi.

Alton Sterling ambaye mauaji yake yaliibua maandamano Marekani
Kipusa huyo anadaiwa kukamatwa na polisi lakini hakuna anayemfahamu wala anayejua kilichomkuta mikononi mwa polisi.

No comments:

Post a Comment