Sunday, 17 July 2016

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa awataka viongozi wazembe wajiondoe


Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deogratius Ndejembi amewaonya watumishi wanaofanya kazi kwa mazoea watafute sehemu nyingine ya kwenda.

Akizungumza katika ufunguzi wa duka la kampuni ya Simu ya Tigo katika mji wa Kibaigwa wilayani Kongwa,  Ndejembe amesema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya kauli mbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ haitawavumilia watendaji wa aina hiyo.

“Nawapa namba ya simu hii mnipigie kwa kero yoyote, nawaahidi nitayafanyia kazi maoni yenu lakini isiwe mambo ya umbeya kwa sababu sitayafanyia kazi hayo,” amesema.

Pia, amewataka wakazi hao kufanya kazi kwa bidii ili kukuza kipato na kuacha kulalamika, kwa sababu maendeleo yanapatikana kwa kufanya kazi siyo  vinginevyo.

No comments:

Post a Comment