Sunday, 10 July 2016

Julius Mtatiro anena kuhusu viongozi wa Siasa za Tanzania


Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro amesema siasa za Tanzania zinakokwenda zinahitaji viongozi wapya, damu tofauti na wanaoweza kutazama mambo kisasa zaidi na kwa mahitaji ya kizazi cha sasa.

Mtatiro amesema jana kuwa  hatarajii kugombea uenyekiti katika chama hicho wala haungi mkono kurejea kwa Profesa Ibrahim Lipumba.

Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari, Mtatiro amesema kwa kipindi kirefu kumekuwa na msukumo mkubwa kutoka kwa viongozi wa chama ngazi za wilaya, wajumbe wa mkutano mkuu, wabunge, madiwani, wanachama, wafuasi na wapenzi wa kada mbalimbali kumtaka ashiriki kinyang’anyiro hicho.

Jana Mwananchi lilikwenda nyumbani kwa Profesa Lipumba ili kujua msimamo wake ndani ya CUF na kuelezwa kuwa amepumzika anajisikia vibaya.

No comments:

Post a Comment