Nyumba 236 zitabomolewa katika Kata ya Makole, Wilaya ya Dodoma mkoani hapa ili kupisha ukarabati na upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Dodoma.
Akizungumza ofisini kwake jana, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana amesema tathmini ilishafanyika kwenye maeneo hayo.
Amewahakikisha wakazi wote watakao takiwa kuhama, hakuna atakaye ondolewa bila kulipwa stahili zake zote za kisheria.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA), Edward Mpanda Amesema mamlaka yake imeshatenga eneo la Ilazo Extension lenye viwanja vilivyopimwa kwa ajili ya wakazi hao.
“Tumepima viwanja 300 katika eneo hilo ambalo litajengwa pia miundombinu mingine,” amesema.
No comments:
Post a Comment