Tuesday, 28 June 2016
Scotland yang'ang'ania kubaki EU
Waziri kiongozi wa Scotland amesema utawala wake utafanya kila linalowezekana kubakia katika Umoja wa Ulaya.
Nicola Sturgeon amesema jana kwamba hatua hizo ni pamoja na uwezekano wa kuzuwia hatua za kisheria zinazohusiana na kujitoa kwa Uingereza kutoka kundi hilo la mataifa.
Wapiga kura wa Scotland wameunga mkono kwa wingi mkubwa kubakia katika Umoja wa Ulaya. Sturgeon pia amesema kura ya pili ya maoni kuhusiana na uhuru wa Scotland kutoka Uingereza pia itajadiliwa.
Amedokeza kwamba kinachomuongoza katika suala hilo ni kulinda maslahi ya Scotland na hasisitizi kuhusu uhuru, lakini iwapo uhuru unakuwa ndio njia pekee ya kulinda maslahi ya Scotland basi itakuwa chaguo litakalojadiliwa.
Labels:
Habari za Kisiasa
Location:
Scotland, Uingereza
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment